BM BARBERSHOP KINONDONI

Saturday, August 18, 2012

SENSA YA WATU NA MAKAZI NI MUHIMU KATIKA MIPANGO YA MAENDELEO - “JIANDAE KUHESABIWA 26 AGOSTI 2012”




Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipitisha Sera ya Taifa ya Idadi ya Watu mwaka 1992. Tangu wakati huo, maendeleo mapya yamekuwa yakitokea kitaifa na kimataifa ambayo yana athari ya moja kwa moja kwenye masuala ya Idadi ya Watu na Maendeleo. Hii imefanya serikali ipitie upya Sera ya Taifa ya Idadi ya Watu ili kujumuisha maendeleo hayo mapya.

Ndani ya nchi, uchumi umebadilika sana kutoka ule uliokuwa ukipangwa na serikali kuu kuwa uchumi wa soko unaozidi kutawaliwa na sekta binafsi, ambayo ina dhima kubwa katika masuala ya idadi ya watu na maendeleo. Zaidi ya hayo, mnamo Juni 1999, serikali ilizindua dira mpya ya maendeleo, yaani, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025. Sera hii iliyodurusiwa, yaani Sera ya Taifa ya Idadi ya Watu ya mwaka 2006 ina lengo la kuratibu na kuhusisha sera, mikakati na programu nyingine ili kuhakikisha maendeleo endelevu ya watu na kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake. Itatekelezwa kwa mkabala jumuishi wa sekta mbalimbali kwa upana zaidi. Aidha,

Serikali itashirikiana na Asasi Zisizo za Serikali (AZISE), sekta binafsi, jumuiya na mawakala wengine wanaotekeleza sera. Kwa hakika, watu binafsi, vyama vya siasa na makundi mengine katika vyama vya kiraia vinatarajiwa kuwa na dhima ya kuhakikisha kufikiwa kwa malengo na madhumuni ya sera. Madhumuni makuu ya dira ya maendeleo ya nchi ni kuwaondoa Watanzania kutoka kwenye umaskini na kuinua ubora wa maisha ya watu. Kwa hiyo, Sera inatoa miongozo ya kushughulikia masuala ya idadi ya watu kwa namna jumuishi.

Hivyo, inatambua mahusiano baina ya mienendo ya idadi ya watu na ubora wa maisha kwa upande mmoja na ulinzi wa mazingira na maendeleo endelevu kwa upande mwingine. Utekelezaji wake utatoa upeo mpya kwa programu za maendeleo kwa kuhakikisha kwamba masuala ya idadi ya watu yanashughulikiwa kikamilifu. Ni matumaini yangu kwamba, kwa kuungwa mkono na kwa ushiriki kamilifu wa watu, utekelezaji wa sera hii utafanikiwa.

Historia ya Sensa Tanzania.
Sensa ya kwanza Tanzania ilifanyika mwaka 1910. Sensa nne za Mwisho zilifanyika baada ya Uhuru, katika miaka ya 1967, 1978, 1988 na 2002. Kulingana na sensa ya mwisho iliyofanyika mwezi Agosti 2002, idadi ya watu nchini Tanzania ilikuwa 34,443,603.

MATOKEO YA SENSA YA WATU 1967-2002 NA MAKADIRIO KATI YA MWAKA 2003-2025 1967-2002 NA MAKADIRIO KATI YA MWAKA
MWAKA            IDADI                 
1967                      12,313,469
1978                      17,512,610
1988                      23,095,885
2002                     34,443,603
IDADI YA KUANZIA MWAKA 2003-2025 MAKISIO
2003                      34,859,582
2004                     35,944,015
2005                     37,083,346
2006                     38,250,927
2009                     41,915,880
2010                      43,187,823
2012                      45,798,475
2015                      49,861,768
2020                     57,102,896
2025                     65,337,918
Maswali yaulizwayo mara kwa mara (Frequently Asked Questions)
Sensa ya Watu na Makazi ni nini?
Jibu la Swali hili-Sensa ya Watu na Makazi ni utaratibu wa kupata na kurekodi habari kuhusu watu na makazi yao.

No comments:

Post a Comment