Mchezaji Mbuyu Twite aliyesajiliwa na Yanga kutoka timu ya FC Lupopo ya DRC aliwasili jana huku Simba Ikiendelea Kumsubiri MBUYI TWITE waliyemsajili kutoka APR ya Rwanda.
Kelele za Twite, Twite zilihanikiza mapokezi ya mchezaji huyu aliyewasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere Milango ya saa kumi jioni jana. Hakika ilikuwa ni furaha, vifijo na nderemo kwa
watu waliofurika kumpokea mchezaji wao mpya Mbuyu Twite.
Mchezaji mpya wa kimataifa wa timu ya taifa ta
Rwanda ,Mbuyu Twite amewasili leo jijini Dar kutokea nchini Rwanda tayari
kujiunga na mabingwa wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati timu ya Young
Africans. Twite aliwsali jana majira ya saa 10:15 kwa majira ya
Afrika Mashariki kwa shirika la ndege la Rwanda Air na kupokelewa na viongozi
wa Young Africans na washabiki wengi waliojitokeza kumpokea Uwanja wa ndege wa
Mwl JK Nyerere. Mara baada ya kuwasili mlango wa kutokea watu
mashuhuri, Twite alipewa jezi ya Yanga yenye namba 4 mgongoni iiiliyoandikwa
jina la Aden Rage, mwenyekiti wa Simba.
Umati mkubwa ulijitokeza kiasi kilichopelekea
Twite kushindwa kutokea mlango wa kawaida wa kupelekea uongozi wa uwanja huo
kumuongoza Twite kutokea mlango wa wageni mashuhuri.
Msafara ulianza Uwanja wa ndege wa Mwl JK Nyerere
kuelekea makao makuu ya klabu, huku magari yakiwa mengi, pikipiki na wengine
wakitembea kwa miguu mpaka makao makuu ya klabu. Mara baada ya kufika
makao makuu ya klabu ya Yanga, mchezaji Mbuyu Twite alipanda juu ghrorofani
kuwasalimia washabiki na wanachama waliojitokeza kumpokea, kisha alikabidhiwa
funguo ya chumba ambacho atakua akikitumia kwa kipindi chote atakachokuwa
Yanga.
Mbuyu Twite amesema anajisikia vizuri, na furaha
na mwenye bahati kuja kuchezea timu ya Yanga na anawaahidi kuonyesha kiwango
cha juu kipindi chake chote atakaoitumikia Young Africans, Twite kesho
anatajumuika na wenzake katika mazoezi asubuhi Uwanja wa Loyola kabla ya
jumamosi kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Coastal Union.
Msafara uliendelea mpaka makao makuu ya klabu,
kwa kupitia mtaa wa msimbazi ambapo wapenzi na washabiki wa simba hawakuweza
kuamini macho yao mara baada ya kumuona Twite akiwa katika gari ndogo ya Yanga,
na washabiki na wanachama wakiwazomea simba na kuwakejeli kwa maneno ya
dhihaka.
Huyo Mbuyu Twite wala sio malikitu mnamshangilia bure tu kwa hiyo staili yake ya nywele. Ngojeni ligi ianze kama ulimi haujawatoka. Safari hii wazee watachukua timu kabla msimu kwisha.
ReplyDelete