BM BARBERSHOP KINONDONI

Sunday, September 23, 2012

FISI AZUA TAFRANI UWANJA WA NDEGE MWANZA


na Sitta Tumma, Mwanza
NDEGE ya Shirika la Precision, juzi ilikwama kwa muda kutua katika uwanja wa ndege wa mjini hapa, baada ya fisi kusimama katikati ya njia ya kurukia na kutua ndege.
Tukio hilo la aina yake limetokea Jumatano wiki hii majira ya saa 2:10 usiku, likihusisha ndege ya kampuni hiyo iliyokuwa ikitokea jijini Dar es Salaam.
Mashuhuda wa tukio hilo walilieleza Tanzania Daima kuwa waliona ndege hiyo ikilazimika kuruka tena juu ghafla ili kumkwepa fisi huyo ambaye hakujulikana alikotokea, jambo ambalo lilileta tafrani kwa abiria.
“Wakati ndege ikianza kutua tulikuwa tunaiona kwa macho yetu. Ghafla tuliiona tena imepaa juu kuelekea ziwani na baadaye ikapita juu ya uwanja ikielekea mashariki,” alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo, meneja wa uwanja wa ndege wa Mwanza aliyetajwa kwa jina moja la Madale, alikiri kuwepo kwa fisi wengi eneo hilo la uwanja na kwamba waliwahi kuuliwa kwa wingi na wanajeshi.
Chanzo: Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment