Wilaya ya Kinondoni ni eneo maarufu ambapo bendi nyingi za
Muziki wa Dansi huwa zinakuwa na maskani huko pamoja na kufanya shughuli zake
za Muziki na kujiimarisha. FM Accademia utawapata Msasani Club, Twanga Pepeta
Utawapata Mango Garden, Extra Bongo Utawapata Sinza Meeda, Acudo Impact
Utawapata Msasani Beach, Mapacha Watatu utawapata Coco Beach, Mashujaa Musica
Utawapata Business Park.
Bendi inayokuja kwa kasi Victoria Sound imeamua kupingana na Usemi huu kwa kuwa na maskani nje ya Kinondoni. Huu unaweza ukawa ni mpango mzuri wa kimapinduzi ambao kama utafanikiwa utaondoa ile dhana kuwa katika jiji la Dar es Salaam, Kila eneo lina aina yake ya Burudani. Mfano ni kama ifuatavyo:
Unapozungumzia Bongo Flava-Basi ujue utaipata kwasana pande za TMK kwa maana ya Temeke na Vitongoji vyake japo si kwamba huku kwenye maeneo mengine haipendwi.
Unapozungumzia Taarabu huwezi kuacha kutaja Ilala na Magomeni. Ukitaka Michiriku hutaiacha Mburtahati, Mbagala na Tandale. Muziki wa Dansi Kinondoni ndiyo Home.
Je Wazo la Bendi Mpya inayokuja kwa Kasi Victoria
Sound Chini ya Meneja Abdulfareed Hussein kupiga nje ya Kinondoni kunaweza kuleta TIJA pamoja na kubadilisha
mazoea yaliyozoeleka kuwa KINOKINO ndiyo Nyumbani kwa Muziki wa Dansi??Lets Wait
No comments:
Post a Comment