Uongozi wa klabu ya yanga
umeshangazwa na kauli ya mwenyekiti wa Simba Alhaji Ismail Aden Rage baada ya
klabu ya Simba kushindwa kumsajili mlinzi wa APR ya Rwanda Mbuyu Twite.
Katibu wa Yanga John Selestine Mwesigwa
amesema Mwenyekiti wa Simba Rage ameshindwa kufanya usajili kwa kwenda na mfumo
wa sasa wakati huu badala yake akitaka kusajili kwa mlango wa nyuma. Kwa mujibu
wa maelezo ya Mwesigwa amesema Yanga ndio waliokuwa wa kwanza kumfuatilia Mbuyi
Twite hata kabla ya kuanza kumfuatilia Kelvin Yondani na Simba ndio waliokuwa
katika mbio za kuizunguka Yanga Jambo ambalo hata hivyo Simba imegonga mwamba.
Mwesigwa amemtaka Mwenyekiti wa
Simba awaambie ukweli wanachama na wapenzi wa klabu yake kilichotokea na vipi
wameshindwa kumsajili mlinzi huyo raia wa DRC badala ya kutupa lawama kwa
uongozi wa Yanga na TFF. Mwesigwa amesema ingekuwa Simba imemsajili kweli Mbuyu
Twite basi mfumo wa kuhamisha wachezaji wa Computer (transfer management system
(TMS) ) ungeonyesha na kukataa data za Yanga kumsajili lakini Simba wakionekana
kutokuwa na taarifa kupitia mfumo huo jambo ambalo mwenyekiti wa Simba
halifahamu na ameshindwa kulielezea hilo.
Katika hatua nyingine Mwesigwa
amesema Yanga haiko tayari kushughulikia madai ya Simba kurejeshwa pesa walizompa
mlinzi huyo kwani wao kama Yanga hawafahamu lolote juu ya hilo.
No comments:
Post a Comment