UFAFANUZI WA PANGO LA MAFISANGO HUU HAPA
Klabu ya Simba ambayo ndiyo mwajiri
wa aliyekuwa kiungo wa klabu hiyo marehemu Patrick Mutesa Mafisango Papaa
imetoa ufafanuzi juu ya kutolewa nje kwa vyombo vya marehemu Mafisango katika
nyumba iliyoko maeneo ya Chang’ombe jijini Dar es salaam.
Afisa habari wa klabu ya Simba Ezekiel
Kamwaga amekiri kuwa ni kweli vyombo vya marehemu Mafisango vilitolewa nje ya
nyumba aliyokuwa anaishi marehemu lakini hilo halihusiani moja kwa moja na
Simba kwasasa kwani wakati vyombo hivyo vinatolewa nje tayari mkataba wa Simba
na mwenye nyumba hiyo ulikuwa umemalizika tangu mwezi wa june 2012.
Kamwaga amesema tangu mkataba huo unamalizika
pango hilo lilikuwa chini ya mdogo wake marehemu ambaye amekuwa akiishi na Mafisango
tangu marehemu akiwa katika klabu ya APR ya Rwanda na baadaye Azam FC kabla ya
kuichezea klabu ya Simba. Mdogo wa marehemu aliomba kuendelea kusalia hapo na
kuendelea kutumia vyombo vya marehemu Mafisango na Simba kwa kutambua udugu na
ukaribu wa wanandugu hao iliamua kumuachia vyombo hivyo lakini kwa makubaliano
ya kutokuendelea kulipa pango hilo mara baada ya mkataba wa nyumba hiyo
kumalizika mwezi wa sita.
Tangu wakati huo mdogo wake na
marehemu aliendelea kuishi katika nyumba hiyo na huku akiwakaribisha ndugu
jamaa na marafiki karibu saba ambao wote ni wa Congo DRC.Taarifa zinasema kuwa
kulikuwa na makubaliano mengine kati ya mwenye nyumba na wakongo hao ambao
mpaka wanatupiwa virago hakukuwa na malipo yoyote yaliyofanyika jambo ambalo
limemfanya mwenye nyumba huyo kushindwa kuendelea kutoa hisani.
No comments:
Post a Comment