BM BARBERSHOP KINONDONI

Sunday, August 5, 2012

IJUE SIRI YA MAFANIKIO YA BAHANUZI KOMBE LA KAGAME


IJUE SIRI YA MAFANIKIO YA BAHANUZI KOMBE LA KAGAME
Saidi Bahanuzi wakati wa Mahojiano


Said Bahanuzi alimaliza michuano ya Kombe la Kagame akiwa na jumla ya mabao sita. Mchezaji huyu ambaye ni mrefu kiasi mweusi na mwili wa kawaida kabisa tofauti na anavyoenekana uwanjani ameelezea historia ya maisha yake katika soka lakini pia akitoa siri nzito ya mafanikio yake katika michuano ya vilabu bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu kama Kombe la Kagame.
Said Bahanuzi akiwa na mwandishi wa habari wa Fatma Likwata Uhuru fm

Mahojiano kati ya Bahanuzi na Uhuru FM yalikuwa kama ifuatavyo:
Mwandishi: Assalam alaykum
Bahanuzi: Alekum msalaam warahmatul taalah- wabarakatul.
Mwandishi: Vipi imepanda lakini?
Bahanuzi: Kama kawaida mi muislam lazima ipande.
Mwandishi: Haya bwana, kubwa hebu tuambie nini siri ya mafanikio yako ndani ya Klabu ya Yanga baada ya muda mfupi wa kujiunga na timu hiyo
Bahanuzi: Siri kubwa ni maombi kwa Mungu lakini pia baraka ambazo zimetokana na  mke wangu kujifungua mototo wa kiume kabla ya michuano ya Kagame hususan siku mbayo nikiwa uwanjani dhidi nya Express ya Uganda mchezo wa kirafiki ambaye nimempa jina la Samir.
Mwandishi: Alaah hongera sana bwana, umempa zawadi gani Samir baada ya michuano hiyo kumalizika?
Bahanuzi: Nilitegemea kumpa zawadi ya kiatu ambacho kingetokana na tuzo ya ufungaji bora lakini mwenyezi mungu hakupenda lakini kwasasa nimempa tuzo yangu ya medali ya ufungaji bora na lile goli la mwisho dhidi ya Azam ni zawadi yake pia
Mwandishi: Kuna tofauti gani kati ya Mtibwa Sugar timu yako ya zamani na Yanga Africans ambayo unaichezea kwasasa?
Bahanuzi: Mtibwa ni timu ndogo lakini Yanga ni timu kubwa kama ilivyo Simba.
Mwandishi: Jina lako limekuwa sasa hasa baada ya Kombe la Kagame kumalizika nini malengo yako?
Bahanuzi: Kwanza ni shukurani kwa Mungu kwakuwa malengo yangu ilikuwa ni kucheza yanga au Simba ambazo ni timu kubwa hapa nchini lakini kucheza timu ya taifa na vilevile kwenda kucheza soka nje ya nchi.
Mwandishi: Wengi wamekuwa wakichanganya juu ya wapi ulikozaliwa. Je ukweli uko wapi maana kuna wengine wanasema wewe ni Mzanzibar na wengine hata wakikuhusisha na kuzaliwa Congo ukweli uko wapi?
Bahanuzi: Hahahahahaaaa mimi ni mtu wa Mwanza lakini nimetokea Kigoma, baba ni mtu wa Kigoma na mama mtu wa Mwanza.

Bahanuzi akimsikiliza kwa makini Limonga Justine katika mahojiano
Mwandishi: Historia yako ikoje katika kandanda
Bahanuzi: Nimeanzia Mwanza ambako ndiko nilikozaliwa na kukulia nilikuwa nacheza mpira mtaani baada ya kumaliza shule. Baadaye nikaja Kibaha kumfuata mama baada ya mama na baba kuachana na baadaye nikaja Dar maeneo ya Ilala lakini muda mwingi nilikuwa Kibaha kwa mama ambako nilikuwa naendelea kucheza timu za mtaani.
Nikiwa kibaha alikuja mtu kutoka Zanzibar alikuwa anatafuta wachezaji kwenda kucheza ligi daraja la pili kule Zanzibar akanichukua nikaenda Zanzibar ligi daraja la pili, ndipo Mtibwa waliponiona wakanifuata nikachezea msimu uliopita kabla ya kuja kucheza Yanga.
Mwandishi:  Kwa maana hiyo wewe ni mtanzania bara?
Bahanuzi: Ya mimi baba yangu ni mtu wa Kasulu Kigoma  na mama mtu wa Mwanza.
Mwandishi: Kumekuwepo na tetesi kuwa wewe ni Mzanzibar, sasa ikitokezea timu za taifa zinachaguliwa na wewe ukapata bahati ya kuchaguliwa utachezea timu ya upande gani Bara au Zanzibar?
Bahanuzi: Mimi ni mtanzania bara nitachezea timu ya bara
Mwandishi: Vipi ushindani katika kikosi cha Yanga ambacho kinawachezaji wengi wazuri lakini wewe umeaminiwa  sana na kocha Thom Saintfiet katika michauno ya Kagame
Mwandishi: Bado sijajua kwasababu licha ya kuaminiwa na kocha lakini ukweli ushindani ni mkubwa sana kwakuwa ndani ya Klabu ya Yanga kuna wachezaji wengi wazuri na wengine nimewakuta na ninawaheshimu, naomba mungu ili nipate namba ya kucheza na sina imani sasa ila naomba mungu inshaalah anisaidie kwa kuwa nina miezi miwili tu katika timu sijui kwa kweli kama nitapata namba .

Bahanuzi akiwa na Kashushu
Mwandishi: Unawaeleza nini wana-Yanga na kwa kuwa hivi sasa ni timu yenye malengo makubwa zaidi ukilanganisha na Mtibwa?
Bahanuzi: Kwa Wana-yanga cha msingi naomba uzima kwasababu ukiwa mzima unaweza kufanya kitu chochote lakini pia kwa Watanzania kama nitaitwa katika timu ya taifa baada ya kuonekana naweza kutoa mchango wangu basi nitafanya kwa kadri mungu anavyotaka kukakamilisha malengo.
Mwandishi: Vipi kuhusu mtoto wako Samiri ambaye umeamua kumpa tuzo ya Kagame unataka afuate nyayo zako kucheza soka?
Bahanuzi:Kwanza apate elimu na baadaye achezea mpira ndio ndoto yangu lakini kwanza elimu
Mwandishi: Sasa umekuwa  na jina kubwa kila sehemu kila mahala ni Bahanuzi redioni, magazetini na kwenye mitandao ya kijamimi ni wewe tu unajisikiaje sasa juu ya hilo?
Bahanuzi : Najisikia vizuri kwa kuwa nafanya kitu kizuri na ni watu ndivo walivyo nipokea kwa hiyo namshukuru mungu na waendelee kunisupport
Mwandishi: Tukirudi uwanjani  umekuwa ukilalamikiwa juu ya kuwa off-side mara kwa mara kiasi kuonekana ndio kasoro kubwa kwako hujui kujipanga kwenye mstari wa off-side hiyo ndio kasoro yako kubwa ukiachana na mambo mengine ya kiufundi unapigiwa filimbi ya off-side unalizungumziaje hilo?
Bahanuzi: Sawa lakini mshambuliaji mzuri lazima apigiwe filimbi ya off-side kwa kuwa unakuwa na uchu wa kufunga magoli.
Mwandishi: Vipi maisha yako mapya ndani ya Yanga unayaonaje?
Bahanuzi: Nashukuru mungu Yanga ni timu nzuri na ninashukuru nina ishi vizuri na wenzangu tunapendana na tunashirikiana lakini vile vile tunasaidiana sana namshukuru mungu sana.
Mwandishi: Vipi kuhusu michuano ya kagame umeionaje?
Bahanuzi:Kagame ilikuwa ni michuano mikubwa kwangu na ilikuwa migumu kwa hiyo kwangu ni historia na kwa kweli imenibadilisha katika misha ya soka na nimejifunza kitu kipya kabisa katika mpira wa miguu.
Mwandishi: Tunashukuru sana baba Samir kwa kututembelea na kupata nafasi ya kuongea na wewe karibu tena endapo tukiwa na lolote tunaomba ushirikiano wako bwana.
Bahanuzi: hahahahahahahaaaaa asante hakuna shaka nakushukuru pia na wewe kwa mahojiano yako.
Mwandishi:  Msalimie mama Samir
Bahanuzi: zimefika

No comments:

Post a Comment