IJUE SIRI YA MAFANIKIO YA BAHANUZI
KOMBE LA KAGAME
Said
Bahanuzi alimaliza michuano ya Kombe la Kagame akiwa na jumla ya mabao sita. Mchezaji huyu ambaye
ni mrefu kiasi mweusi na mwili wa kawaida kabisa tofauti na anavyoenekana
uwanjani ameelezea historia ya maisha yake katika soka lakini pia akitoa siri
nzito ya mafanikio yake katika michuano ya vilabu bingwa Afrika Mashariki na Kati
maarufu kama Kombe la Kagame.
Said
Bahanuzi akiwa na mwandishi wa habari wa Fatma Likwata Uhuru fm
|
Mahojiano
kati ya Bahanuzi na Uhuru FM yalikuwa kama ifuatavyo:
Mwandishi:
Assalam alaykum
Bahanuzi: Alekum msalaam warahmatul taalah-
wabarakatul.
Mwandishi: Vipi imepanda lakini?
Bahanuzi: Kama kawaida mi muislam lazima
ipande.
Mwandishi: Haya bwana, kubwa hebu tuambie nini
siri ya mafanikio yako ndani ya Klabu ya Yanga baada ya muda mfupi wa kujiunga
na timu hiyo
Bahanuzi: Siri kubwa ni maombi kwa Mungu
lakini pia baraka ambazo zimetokana na mke wangu kujifungua mototo wa
kiume kabla ya michuano ya Kagame hususan siku mbayo nikiwa uwanjani dhidi nya
Express ya Uganda mchezo wa kirafiki ambaye nimempa jina la Samir.
Mwandishi:
Alaah hongera
sana bwana, umempa zawadi gani Samir baada ya michuano hiyo kumalizika?
Bahanuzi: Nilitegemea kumpa zawadi ya kiatu
ambacho kingetokana na tuzo ya ufungaji bora lakini mwenyezi mungu hakupenda
lakini kwasasa nimempa tuzo yangu ya medali ya ufungaji bora na lile goli la
mwisho dhidi ya Azam ni zawadi yake pia
Mwandishi:
Kuna tofauti gani
kati ya Mtibwa Sugar timu yako ya zamani na Yanga Africans ambayo unaichezea
kwasasa?
Bahanuzi: Mtibwa ni timu ndogo lakini Yanga ni
timu kubwa kama ilivyo Simba.
Mwandishi:
Jina lako limekuwa
sasa hasa baada ya Kombe la Kagame kumalizika nini malengo yako?
Bahanuzi: Kwanza ni shukurani kwa Mungu
kwakuwa malengo yangu ilikuwa ni kucheza yanga au Simba ambazo ni timu kubwa
hapa nchini lakini kucheza timu ya taifa na vilevile kwenda kucheza soka nje ya
nchi.
Mwandishi:
Wengi wamekuwa
wakichanganya juu ya wapi ulikozaliwa. Je ukweli uko wapi maana kuna wengine
wanasema wewe ni Mzanzibar na wengine hata wakikuhusisha na kuzaliwa Congo
ukweli uko wapi?
Bahanuzi: Hahahahahaaaa mimi ni mtu wa
Mwanza lakini nimetokea Kigoma, baba ni mtu wa Kigoma na mama mtu wa Mwanza.
Bahanuzi
akimsikiliza kwa makini Limonga Justine katika mahojiano
Mwandishi:
Historia yako
ikoje katika kandanda
Bahanuzi: Nimeanzia Mwanza ambako ndiko nilikozaliwa
na kukulia nilikuwa nacheza mpira mtaani baada ya kumaliza shule. Baadaye
nikaja Kibaha kumfuata mama baada ya mama na baba kuachana na baadaye nikaja
Dar maeneo ya Ilala lakini muda mwingi nilikuwa Kibaha kwa mama ambako nilikuwa
naendelea kucheza timu za mtaani.
Nikiwa
kibaha alikuja mtu kutoka Zanzibar alikuwa anatafuta wachezaji kwenda kucheza
ligi daraja la pili kule Zanzibar akanichukua nikaenda Zanzibar ligi daraja la
pili, ndipo Mtibwa waliponiona wakanifuata nikachezea msimu uliopita kabla ya
kuja kucheza Yanga.
Mwandishi:
Kwa maana hiyo wewe ni mtanzania bara?
Bahanuzi: Ya mimi baba yangu ni mtu wa Kasulu
Kigoma na mama mtu wa Mwanza.
Mwandishi:
Kumekuwepo na
tetesi kuwa wewe ni Mzanzibar, sasa ikitokezea timu za taifa zinachaguliwa na
wewe ukapata bahati ya kuchaguliwa utachezea timu ya upande gani Bara au
Zanzibar?
Bahanuzi: Mimi ni mtanzania bara nitachezea
timu ya bara
Mwandishi:
Vipi ushindani
katika kikosi cha Yanga ambacho kinawachezaji wengi wazuri lakini wewe
umeaminiwa sana na kocha Thom Saintfiet katika michauno ya Kagame
Mwandishi:
Bado sijajua kwasababu
licha ya kuaminiwa na kocha lakini ukweli ushindani ni mkubwa sana kwakuwa
ndani ya Klabu ya Yanga kuna wachezaji wengi wazuri na wengine nimewakuta na
ninawaheshimu, naomba mungu ili nipate namba ya kucheza na sina imani sasa ila
naomba mungu inshaalah anisaidie kwa kuwa nina miezi miwili tu katika timu
sijui kwa kweli kama nitapata namba .
Bahanuzi
akiwa na Kashushu
Mwandishi:
Unawaeleza nini
wana-Yanga na kwa kuwa hivi sasa ni timu yenye malengo makubwa zaidi
ukilanganisha na Mtibwa?
Bahanuzi:
Kwa Wana-yanga
cha msingi naomba uzima kwasababu ukiwa mzima unaweza kufanya kitu chochote lakini
pia kwa Watanzania kama nitaitwa katika timu ya taifa baada ya kuonekana naweza
kutoa mchango wangu basi nitafanya kwa kadri mungu anavyotaka kukakamilisha
malengo.
Mwandishi:
Vipi kuhusu mtoto
wako Samiri ambaye umeamua kumpa tuzo ya Kagame unataka afuate nyayo zako
kucheza soka?
Bahanuzi:Kwanza apate elimu na baadaye achezea
mpira ndio ndoto yangu lakini kwanza elimu
Mwandishi:
Sasa
umekuwa na jina kubwa kila sehemu kila mahala ni Bahanuzi redioni,
magazetini na kwenye mitandao ya kijamimi ni wewe tu unajisikiaje sasa juu ya
hilo?
Bahanuzi
: Najisikia vizuri
kwa kuwa nafanya kitu kizuri na ni watu ndivo walivyo nipokea kwa hiyo
namshukuru mungu na waendelee kunisupport
Mwandishi: Tukirudi uwanjani umekuwa
ukilalamikiwa juu ya kuwa off-side mara kwa mara kiasi kuonekana ndio
kasoro kubwa kwako hujui kujipanga kwenye mstari wa off-side hiyo ndio
kasoro yako kubwa ukiachana na mambo mengine ya kiufundi unapigiwa filimbi ya off-side
unalizungumziaje hilo?
Bahanuzi: Sawa lakini mshambuliaji mzuri lazima
apigiwe filimbi ya off-side kwa kuwa unakuwa na uchu wa kufunga magoli.
Mwandishi:
Vipi maisha yako
mapya ndani ya Yanga unayaonaje?
Bahanuzi: Nashukuru mungu Yanga ni timu nzuri
na ninashukuru nina ishi vizuri na wenzangu tunapendana na tunashirikiana
lakini vile vile tunasaidiana sana namshukuru mungu sana.
Mwandishi:
Vipi kuhusu
michuano ya kagame umeionaje?
Bahanuzi:Kagame ilikuwa ni michuano mikubwa
kwangu na ilikuwa migumu kwa hiyo kwangu ni historia na kwa kweli
imenibadilisha katika misha ya soka na nimejifunza kitu kipya kabisa katika
mpira wa miguu.
Mwandishi:
Tunashukuru sana
baba Samir kwa kututembelea na kupata nafasi ya kuongea na wewe karibu tena
endapo tukiwa na lolote tunaomba ushirikiano wako bwana.
Bahanuzi:
hahahahahahahaaaaa
asante hakuna shaka nakushukuru pia na wewe kwa mahojiano yako.
Mwandishi:
Msalimie mama Samir
Bahanuzi: zimefika
No comments:
Post a Comment