BM BARBERSHOP KINONDONI

Sunday, August 5, 2012

JUMA KASEJA JUMA ADHIBITISHA KUWA ANATUMIA NDUMBA


Golikipa anayetumainiwa na Klabu ya Simba ya Dar es Salaam pamoja na timu ya Taifa Stras Juma Kaseja Juma maarufu kama TANZANIA ONE amedhihirisha kuwa yeye anaishi kwa kutegemea UCHAWI, NDUMBA au TUNGULI katika kufanikisha malengo yake kwenye kazi yake iliyomtoa nyumbani kwao Kigoma yaani Mpira. Tukio hili limetokea kufuatia uthibitisho wa fulana aliyovaa kwenye moja ya Mechi kwenye Uwanja Mpya wa Taifa Maarufu Kama UWANJA MKUBWA. Alipoulizwa kwanini amefanya hivyo alijibu kuwa: Kwakuwa ninaandamwa na baadhi ya Magolikipa wenzangu kuwa mimi natumia NDUMBA kwenye mpira ndiyo maana nimeona niwadhihirishie kuwa hilo lina ukweli ndani yake. Miongoni mwa Magilikipa ambao Juma Kaseja amewahi kudakia nao timu moja ni Pamoja na Golikipa aliyehamia Yanga mwaka huu kutokea Simba Ally Mustafa Bartez ambaye baada ya kujiunga na Yanga ameonyesha umahili wake kwenye mechi za Kombe la Kagame na kufanikiwa kuiwezesha timu ya Yanga kunyakua Ubingwa wa Kagame bila yeye Bartez kufungwa Goli hata Moja.
JUMA KASEJA JUMA NA FLANA YAKE YENYE MAANDISHI YALIYOANDIKWA (ndumba asili yangu kuna ubishi?)

No comments:

Post a Comment