MSHAMBULIAJI hatari wa Timu ya Yanga aliye kwenye chati kwa sasa,
Said Bahanuzi amefanyiwa kitu mbaya katika mtandao wa kijamii maarufu kama
Facebook. Mwanandinga huyo alipatwa na masahibu hayo kufuatia mtu asiyejulikana
kufungua akaunti kwa kutumia jina la straika huyo hatari na kuanza kuwasiliana
na watu mbalimbali ambapo wengi walikuwa wakiamini wanawasiliana na Bahanuzi.
Akichezesha taya na Udaku Spoti, Bahanuzi alisema hajawahi
kujihusisha na masuala ya Facebook na kusema hajui lolote juu ya mtandao huo
lakini amemlaani vikali mtu huyo anajifanya ni Bahanuzi kwani anamchafulia.
No comments:
Post a Comment