BM BARBERSHOP KINONDONI

Tuesday, October 2, 2012

SEGERA YAGEUKA RANGI NYEKUNDU BAADA YA BASI LA DAR EXPRESS KUUNGUA MOTO

 
Basi la Kampuni ya Dar express linalofanya safari zake kati Dar Es Salaam na Arusha limeteketea kwa mot oleo eneo la Segera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga. Kwa mujibu wa habari zilizoifikia Mwanatanga ni kwamba zahama hiyo ilitokea muda mfupi baada ya basi hilo kusimama eneo hilo maarufu la Segera ambayo ni njia panda ya Tanga , Dar es Salaam na Arusha.

Mbali na moto huo kuteketeza kabisa basi hilo hakuna majeruhi wala aliyepoteza maisha kufuatia ajali hiyo mbaya.  Aidha mwanatanga inadhani ni wakati muafaka sasa kwa wenye Mabasi pamoja na Mamlaka kuchukua tahadhari za Kiukaguzi kabla ya mabasi hayo kuanza Safari ili kuweza kuepusha ajali ambazo zinaweza kuepukika. Jumla ya abiria wapatao 65 wamenusurika kufuatia ajali hiyo. Picha za tukio zima hizi hapa.





No comments:

Post a Comment