MCD akicharaza Tumba |
BENDI ya muziki wa Dansi nchini
Mashujaa imetanabahisha kuwa mwanamuzi wake MCD aliyerejea kwenye Bendi yake ya
zamani Twanga Pepeta alikuwa akirudisha nyuma maendeleo ya Bendi hizo kutokana
na sababu mbalimbali kama zifuatazo:
1.
Mpiga
Tumba huyo alikuwa na tatizo la kutowaamini wenzake
2.
Alikuwa
anapenda kupanga upya sauti kila anapopanda yeyé jukwaani kazi ambayo huifanya
kwa zaidi ya saa nzima huku wapenzi wakisubiri muziki.
3.
Alikuwa
na tabia ya kubomoa na kuvipanga upya vyombo hata kama wenzake walikuwa
wakiendelea kutoa burudani
4.
Pamoja
na nafasi kubwa aliyopewa kutokana na heshima na umri wake lakini bado alikuwa
ni mchelewaji nambari moja kazini na kutoa sababu zisizotosheleza
Tabia hizi zilikuwa ni kero kwa wanamuziki
wenzake pamoja na Washabiki kwa ujumla.
Chanzo cha habari hii ni. Gazeti la Dimba
Jumatano Aprili 10-13 TOLEO NA. 2718
No comments:
Post a Comment