KUANZA KWA MJI
WA DAR ES SALAAM
Maumbile ya ardhi ya eneo la jiji la Dar es salaam yamegwanyika
katika sura kuu nne.Upande wa mashariki kuna ufuko wa bahari unaoinuka hadi
m.50 juu ya usawa wa bahari ukifuatiwa na uwanda wa chini wa pwani wenye
mwinuko mdogo wa m.50-100 juu ya usawa wa bahari.Magahribi mwa ukanda huu,kuna
vilima vya Pugu ,vyenye miinuko kati ya m.100 na m.350 juu ya usawa wa bahari
na vimekatishwa na mabonde ya mito yenye miteremko mikali inayoelekeza maji
yake kwenye bahari ya Hindi.Baadhi ya mito hiyo ni mto Msimbazi huingia
baharini kupitia kwenye ghuba yenye tingatinga za mimea aina ya mikoko.
Hali ya hewa ya Dar es salaam ni ya joto kama ilivyo
kawaida kwa maeneo ya pwani ya tropiki ambapo wastani wa kiwango cha unyevu
katika hewa ni wa juu asilimia 96 nyakati za asubuhi na asilimia 67 nyakati za
alasiri. Wastani wa mvua kwa mwaka ni milimita 1,000. Chimbuko la Jiji la Dar
es salaam ni uamuzi uliofanywa na Sultani Majid bin Said wa Zanzibar mwaka
1862,na kujenga makao yake mapya pamoja na bandari katika Pwani ya Tanganyika. Lengo
la uamuzi huo ilikuwa ni kuimarisha njia za biashara 'Carravan' zilizofunguliwa
kuelekea kwenye maeneo ya Afrika Mashariki na ambazo zilijulikana kama 'Caravan
Routes'. Ujenzi wa makao ya Sultani pamoja na bandari ulianza rasmi mwaka 1865
katika eneo la kijiji kidogo kilichojulikana kwa jina la Mzizima.Ujenzi huo
ulikamilika mwaka 1866 na Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es salaam mwaka
huo.
Mara baada ya kuanzishwa, mji wa Dar es salaam ulipanuka na
uchumi wake kukua kwa kasi kubwa ingawaje ni kwa kipindi kifupi tu hadi Sultani
Majid bin Said alipokufa mwaka 1870. Kifo cha Sultani huyo kilisababisha
kudidimia kwa maendeleo ya mji wa Dar es salaam. Hali hiyo ilianza tena
kubadilika mwaka 1884 kufuatia kuanzishwa kwa koloni la Wajerumani la Afrika ya
Mashariki.
![]() | |
UKUMBI WA KARIMJEE DAR ES SALAAM |
Mwaka 1891 serikali ya kikoloni ya Kijerumani iliamua
kuhamisha makao makuu ya utawala wao katika Afrika Mashariki Bagamoyo na
kuyaweka Dar es salaam. Hata baada ya Wajerumani kushindwa na Waingereza katika
vita kuu ya kwanza ya dunia mwaka 1916,mji wa Dar es salaam uliendelea kuwa
makao makuu ya utawala wa koloni la Waingereza nchini Tanganyika,hadi
Tanganyika ilipopata uhuru wake mwaka 1961. Dar es salaam iliendelea kuwa makao
makuu ya Tanganyika huru na hatimaye kuwa makao makuu ya Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania hadi mwaka 1972 wakati serikali ilipoamua kuhamishia makao
yake makuu mjini Dodoma.
Mji wa Dar es salaam ulitangazwa kuwa mji wenye serikali
yake ya mtaa mwaka 1920. Hadhi ya mji wa Dar es salaam ilipandishwa kuwa
manispaa mwaka 1949 na baadaye kutunukiwa hadhi ya Jiji la Malkia wa himaya ya
Uingereza, wakati Tanganyika ilipopata uhuru mwaka 1961. Kwa kipindi hicho,Jiji
la Dar es salaam lilikuwa likiongozwa na halmashauri ya Jiji la Dar es salaam
hadi mwaka 1972 wakati ambapo serikali ilivunja serikali zote za mitaa nchini
ili kutekeleza mfumo wa madaraka mikoani.Mamlaka za miji nchini Tanzania
zilirejeshewa madaraka mwaka 1978.
Mwaka 1857 mji wa Dar es salaam ulikuwa na watu 3,000 tu.Idadi hiyo iliongezeka hadi kufikia watu 128,742 mwaka 1957,watu 272,821 mwaka wa 1967.Idadi ya wakazi wa Dar es salaam kwa mujibu wa sensa,ilikuwa 843,000 mwaka 1978 na kuongezeka hadi kufikia watu 1,360,850 mwaka 1988.
Idadi ya watu kwa sasa Jijini Dar es salaam inakadiriwa
kufikia zaidi ya 3,000,000 kukiwa na mamlaka za manispaa katika wilaya za Ilala,
Kinondoni na Temeke. Ongezeko hili la watu ndani ya Jiji la Dar es salaam na
manispaa zake linazua changamoto katika uwekezaji zaidi kwenye miundo mbinu ya
huduma za kijamii katika sekta za afya, elimu, mazingira na usafirishaji. Mawakala
wa huduma za forodha ni sehemu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na huduma zao
zinaendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii Jijini Dar es Salaam
na Tanzania kwa ujumla.
Mkoa wa Dar es Salaam ulianzishwa kutoka Mkoa wa Pwani
ukiwa na Wilaya 3 za Ilala, Kinondoni na Temeke. Kipindi hicho Serikali kuu
ilihodhi madaraka. (Madaraka Mkoani) Mfumo wa Serikali za Mitaa ulirejeshwa
tena mwaka 1982-1984. Hata hivyo Mamlaka za Serikali za Mitaa za Mkoa wa Dar es
Salaam zilizopo sasa zilianzishwa mwaka 2000 baada ya kuvunjwa iliyokua Tume ya
Jiji iliyokuwepo tangu 1996 hadi 1999. Hadi sasa mwaka 2012 Mkoa wa Dar e s
Salaam una Wilaya 3 za kiutawala Ilala, Kinondoni na Temeke ambazo pia ni
Halmashauri za Manispaa, pia ipo Halmashauri ya Jiji na Majimbo 8 ya uchaguzi
Tarafa 10, Kata 90 na Mitaa 448.
HISTORIA YA
MKOA WA DAR ES SALAAM
![]() |
JENGO LA HALMASHAURI YA JIJI LA DAR ES SALAAM |
Kabla ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 Mkoa wa Dar es
Salaam haukuwepo, kilichokuwepo ni mji wa Dar es Salaam. Mkoa ulianzishwa mwaka
1974 wakati wa madaraka mikoani. Jina la Dar es salaam lilitokana na majilio ya
wageni wa Kiarabu, waliotokea pande za Persia. Waliita (Bandari Ur Salama) Kwa
lugha ya Kiswahili Bandari ya Salama. Kihistoria, Jiji hili limekaliwa na
kutawaliwa na wageni wa aina mbalimbali. Dar es Salaam ilipata hadhi ya mji
mdogo mwaka 1920 na mwaka 1949 ilipata hadhi ya kuwa Manispaa.
Miaka ya Sitini Mkoa wa Dar es Salaam uligawanywa kwenye
Maeneo Makuu matatu ya Kinondoni, Temeke na Ilala ikiwa chini ya Wilaya ya Mzizima.
Magawnyo huu uliwezesha wakazi wa maeneo hayo matatu kuwa na shughuli tofauti
za kiuzalishaji mali kulingana na maeneo wanayotoka.
HISTORIA YA
MANISPAA YA KINONDONI
![]() |
JENGO LA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI |
Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ina ukubwa wa kilomita
za mraba 531. Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imepakana na Wilaya ya
Bagamoyo upande wa Kaskazini, upande wa Kaskazini Mashariki inapakana na Bahari
ya Hindi, upande wa Kusini inapakana na Manispaa ya Ilala, upande wa Kusini
Magharibi inapakana na Wilaya ya Kisarawe na upande wa Magharibi inapakana na
Wilaya ya Kibaha.
HISTORIA YA MANISPAA YA TEMEKE
![]() |
JENGO LA HALMASHAURI YA MANISPAA YA TEMEKE |
Kabla ya Uhuru mwaka 1961 Wilaya ya Temeke ilikuwa katika
mkoa wa Pwani. Miaka ya 1980 ilihamishiwa mkoa wa Dar Es Salaam. Watu wa Temeke kabla ya Uhuru wengi wao walikuwa
wazawa kwa maana ya Wazaramo, Wandengereko, Wakwere na Wamakonde wachache. Halmashauri
ya Manispaa ya Temeke ilianzishwa rasmi tarehe 1/2/2000. Asili ya Wakazi wa
Temeke niwacheza bao na Ngoma za asili, mchezo wa bao ulikuwa ukichezwa kwenye
maeneo maarufu kule Temeke hususan Mwembeyanga, Mwembemkamba na African Temeke.
Ngoma kama Vile Tokomile, Mkwaju Ngoma, Mganda, Gombesugu, Mchunje,
Mchape, Mtondoo, Buti, Msewe Inayotambulika kama ngoma ya Mangariba zilichezwa
sana eneo hili lililokuwa mkoa wa Pwani hapo awali. Vikundi maarufu wakati huo kwenye
suala la ngoma moja wapo ni kikundi cha NGASUMO kilichokuwa kikipiga ngoma ya
Tokomile maeneo ya Tandika sokoni. Aidha
Mangariba maarufu walikuwa LUMALIZA aliyeishi kati ya mtaa wa Ruvuma na Madenge
na wengine ni SINDE, NZASA na SUBA taarifa hii nikwamujibu wa Mzee Shaaban Mzee
Marufui sana eneo la Temeke Wailes.
Halimashauri ya Manispaa ya Temeke ni kubwa kieneo kuliko
Manispaa zote ikiwa na eneo la kilomita za mraba 656; ipo upande wa kusini wa
Mkoa wa Dar es Salaam ambapo kwa upande wa mashariki inapakana na Bahari ya
Hindi, kusini inapakana na Wilaya ya Mkuranga – Mkoa wa Pwani na upande wa
kaskazini na magharibi inapakana na Manispaa ya Ilala.
HISTORIA YA MANISPAA YA ILALA
![]() |
JENGO LA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA |
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ipo kati ya Latitudo 6 na
7 kusini mwa Ikweta na kati ya Longitudo 39 na 40 Mashariki. halmashauri ya
Manispaa ya Ilala ina eneo la kilomita za mraba 210 ambapo zaidi ya asilimia
75% ya eneo hilo la Manispaa ya Ilala ni eneo la mji.
Manispaa ya Ilala imepakana na Manispaa za Kinondoni na Temeke kwa upande wa Kaskazini na Kusini, Mkoa wa Pwani kwa upande wa Magharibi na Bahari ya Hindi katika ukanda wa Pwani wenye urefu Kilomita 10 kwa upande wa Mashariki. Idadi ya Watu Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002, Manispaa ya Ilala ilikuwa na wakazi 637,573 wakiwemo Wanaume 321,903 sawa na asilimi 50.5% na Wanawake 315,670 sawa asillimi 49.5. Ongezeko la watu ni asilimia 4.6 kwa mwaka, Hivyo inakadiriwa kuwa idadi ya watu imefikia 795,024 mwaka 2007.
Manispaa ya Ilala ina jumla ya Kaya 187,581. Wastani wa ukubwa wa Kaya ni watu
4.3.
Manispaa ya Ilala imepakana na Manispaa za Kinondoni na Temeke kwa upande wa Kaskazini na Kusini, Mkoa wa Pwani kwa upande wa Magharibi na Bahari ya Hindi katika ukanda wa Pwani wenye urefu Kilomita 10 kwa upande wa Mashariki. Idadi ya Watu Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002, Manispaa ya Ilala ilikuwa na wakazi 637,573 wakiwemo Wanaume 321,903 sawa na asilimi 50.5% na Wanawake 315,670 sawa asillimi 49.5. Ongezeko la watu ni asilimia 4.6 kwa mwaka, Hivyo inakadiriwa kuwa idadi ya watu imefikia 795,024 mwaka 2007.
BANDARI YA DAR ES SALAAM INAUWEZO MKUBWA |
Wilaya ya Ilala inamezwa sana na Jiji kwakuwa pale ndiyo
sehemu ambayo waliishi watu wenye asili ya Weupe. Maeneo ya Halmashauri ya
Ilala yalijigawa kwa mabaka ya weupe kama ifuavyo:
Eneo la Kariakoo (Gerezani) waliishi waarabu wengi hadi
maeneo ya karibu na Ilala Boma kuanzia pale Shauri Moyo. Eneo la Sokoni
Kariakoo, Rumumba lilikuwa na Wapagazi wengi waliokuwa wanabeba mizigo
inayotoka Bandarini wakati huo kwa kuja na Majahazi kutoka Zanzibar, Tanga,
Shelisheli, Bagamoyo na Mashariki ya Mbali.
IDADI YA WATU
Mwaka 1948 mji wa Dar es Salaam ulikuwa na watu wapatao
69,227. Idadi ya watu imekuwa ikiongezeka kwa asilimia 4.3 (sensa ya 2002), hivyo
sensa ya 2002 idadi ya watu ilifikia 2,497,000. Hadi sasa mwaka 2012 Jiji la
Dar es Salaam linakadiriwa kuwa na watu 3,118,132 mabadiliko ya kisensa
yanatarajiwa baada ya Sensa hii ya mwaka 2012.
UTAWALA
Kabla ya ukoloni walitawala Machifu na wazee wa mila.
Walipokuja wakoloni walijitahidi kupambana na utawala huo na baada ya uhuru utawala wa machifu uliondolewa, wakoloni
walifanya kazi na Serikali za Mitaa ambazo zilivunjwa baadae.
MIUNDOMBINU
Mwaka 1961 ukubwa wa eneo la Dar es Salaam wakati huo
ilikuwa kilometa za mraba 635 na sasa Jiji la Dar es Salaam lina eneo la
kilometa za mraba 1,397. Kuhusu utoaji hati za umiliki wa ardhi iuikua
unafanyika makao makuu ya Wizara pekee, kwa sasa kuna kanda zimeanzishwa ambapo
hati hutolewa huko. Usafiri wa umma umekua kutoka treni na mabasi hadi ndege,
meli/boti kwa sasa.
FUATANA NAMI KESHO KWENYE UJUE USAFITRI WA UMMA ULIKOANZIA JIJINI DAR ES SALAAM!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
KESHO - SCENE NO. 2 – Historia ya Usafiri wa Umma Jiji la Dar Es Salaam
No comments:
Post a Comment