Mkali wa drum anayeing'arisha Twanga Pepeta alimshangaza
sana Ally Choki kwa uwezo wake mwanafunzi huyu wa Petit Makambo na Hamisi
Magendela na Baadaye kukomazwa na marehemu Abuu Ally Semhando.
James Michael Kibosho anasimulia historia yake
kwenye Muziki kama ifuatavyo:
"NILIANZA kuchezo shoo katika kumbi mbalimbali za starehe na kwenye shughuli ikiwemo maharusi kabla ya kupiga 'drums' ambayo ndiyo ilikuwa ndoto yangu kubwa maishani mwangu".
Hivi ndivyo alivyoanza kujieleza mpiga vyombo huyo tegemeo wa bendi ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twanga Pepeta', James Michael almaarufu 'Kibosho', jina la ukoo wao.
"NILIANZA kuchezo shoo katika kumbi mbalimbali za starehe na kwenye shughuli ikiwemo maharusi kabla ya kupiga 'drums' ambayo ndiyo ilikuwa ndoto yangu kubwa maishani mwangu".
Hivi ndivyo alivyoanza kujieleza mpiga vyombo huyo tegemeo wa bendi ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twanga Pepeta', James Michael almaarufu 'Kibosho', jina la ukoo wao.
Mwanamuziki huyu ambaye kwa sasa anabeba jahazi
katika upande wa kucharaza mabati hayo, ambayo yanakuwa ni muongozo kwenye
upigaji wa vyombo, anasema anajisikia faraja kufikia hatua hiyo baada ya safari
ndefu yenye vikwazo vingi. Nyota huyu ambaye ni mtoto wa tano katika ya watoto
watano wa Mzee Michael Kibosho, anasema baada ya kumaliza elimu ya msingi 2001,
katika shule ya msingi Umoja iliyopo Mabibo, Dar es Salaam, Manispaa ya
Kinondoni, na baadaye kuingia rasmi kwenye miziki. Anasema mwaka 2002 alianza
kujifunza kupiga 'drums' katika bendi ya Lolita. Kutokana na kiu ya kupenda
fani hiyo aliweza kujua kwa haraka sana na kuanza kupiga katika bendi
zilizokuwa zikipiga muziki kwenye kumbi kwa ujira wa sh 1500 hadi 2000 kwa
siku. "Kupiga drums katika bendi hizo nilipata ujuzi wa kutosha na
kufanikiwa kujiunga katika bendi ya Maliki Star iliyokuwa ikiongozwa na Petit
Makambo, ambaye alinipa mafunzo zaidi ya kutumia chombo hicho ambacho sasa
napata riziki. Kwa kweli alinipa siri kubwa ambayo naitumia na kuwa tofauti na
wapiga 'drums' wengine na hadi leo namheshimu sana,"
Kibosho anasema baada ya kipindi kifupi,
alikwenda Jijini Tanga kuanzisha bendi ya Super Sound, chini ya Makambo. Mapema
2003 wakaja Dar es Salaam kurekodi nyimbo kadhaa ambazo zilikuwa zimekamilika
baada ya kukaa kambini Jijini Tanga kwa muda wa miezi sita. James anabainisha
kuwa baada ya kumaliza kurekodi nyimbo mbalimbali, walirejea Jijini Tanga.
Kibosho alisikia kuwa kuna bendi mpya inayoitwa Extra Bongo ikiwa chini ya
'Mzee wa Farasi', Alli Choki, ndipo akapata ushawishi wa kwenda Dar es Salaam
kujaribu bahati yake.
"Ilikuwa kawaida yangu kujaribu kila eneo nililohisi kuwa na mafanikio japo ilikuwa kawaida yangu kununua kanda za kaseti na kusikiliza na kuzifanyia mazoezi kitu ambacho kiliniwezesha kujua mapigo ya nyimbo mbalimbali tofauti," anaweka wazi Kibosho.
"Ilikuwa kawaida yangu kujaribu kila eneo nililohisi kuwa na mafanikio japo ilikuwa kawaida yangu kununua kanda za kaseti na kusikiliza na kuzifanyia mazoezi kitu ambacho kiliniwezesha kujua mapigo ya nyimbo mbalimbali tofauti," anaweka wazi Kibosho.
Mwanamuzki huyu anasema aliweza kununua kaseti ya albamu ya Extra Bongo ya 3X3 kwa lengo la kupata uzoefu kabla ya kwenda Dar es Salaam kujaribu bahati yake.
Baada ya kufanya mazoezi ya kutosha na kujiridhisha kuwa amefikia kiwango cha kutosha, alinyanyua mguu nakwenda Dar es Salaam na kuomba nafasi ya kujaribiwa kupiga kifaa hicho. "Nilikutana na Mkurugenzi wa bendi Ally Choki, baada ya kuzungumza naye alinijaribu kwenye kupiga drums kwa hakika nilifanya maajabu 'wonders', kila mmoja alikubali uwezo wangu baada ya kupiga kibao cha 3X3," alisema J Kibosho.
Baada ya miezi mitatu aliitwa na uongozi wa bendi
hiyo na kutambulishwa rasmi kupigia bendi ya Extra Bongo. Nilijisikia faraja
kuwemo katika kikosi kazi cha bendi hiyo nikiamini kuwa ulikuwa mwanzo wa
kuonekana kuelekea kwenye mafanikio kupitia tasnia hiyo," anasema.
Mwanamuziki huyo aliyezaliwa Desemba 17, 1987 Jijini Dar es Salaam anasema baada ya kuingia katika bendi hiyo alifanikiwa kupiga nyimbo kadhaa ikiwemo ya Double Double iliyofanya vizuri katika maeneo mbalimbali na baada ya siku chache kundi hilo lilivunjika na kujiunga Double Extra iliyokuwa chini ya Mwinjuma Muuni na Alli Choki 'Mzee wa Farasi' na kwenda Chalinze kukaa kwa miezi miwili kabla ya kutoa albamu ya kwanza iliyopewa jina la Chungeni Ndoa.
Mwanamuziki huyo aliyezaliwa Desemba 17, 1987 Jijini Dar es Salaam anasema baada ya kuingia katika bendi hiyo alifanikiwa kupiga nyimbo kadhaa ikiwemo ya Double Double iliyofanya vizuri katika maeneo mbalimbali na baada ya siku chache kundi hilo lilivunjika na kujiunga Double Extra iliyokuwa chini ya Mwinjuma Muuni na Alli Choki 'Mzee wa Farasi' na kwenda Chalinze kukaa kwa miezi miwili kabla ya kutoa albamu ya kwanza iliyopewa jina la Chungeni Ndoa.
Mwaka 2004 bendi hiyo ilivunjika na yeye kujiunga
na bendi ya Double M Sound akiwa chini ya Muumini 'Kocha wa Dunia', na wakafanikiwa
kutoa albamu ya Titanic iliyokuwa na nyimbo saba na kufanikiwa kupiga nyimbo
sita ikiwemo Ukewenza, Titanic, Ndoa ya Ufukara, Mapenzi Siyo Mtaji, Air Omani
ambayo haikufanya vizuri katika soko la muziki.
"Unajua kutokana na matatizo madogo bendi ilivunjika nikajiunga na Mchinga Sound 'G8' ambayo nilidumu nayo kwa wiki moja tu ndipo nikapata nafasi ya kujiunga African Stars 'Twanga Pepeta' na kupokelewa tena na Ally Choki Mzee Wa Farasi baada ya kufaulu kupiga vyema kibao cha Safari 2005," anasema.
"Unajua kutokana na matatizo madogo bendi ilivunjika nikajiunga na Mchinga Sound 'G8' ambayo nilidumu nayo kwa wiki moja tu ndipo nikapata nafasi ya kujiunga African Stars 'Twanga Pepeta' na kupokelewa tena na Ally Choki Mzee Wa Farasi baada ya kufaulu kupiga vyema kibao cha Safari 2005," anasema.
Baada ya kufika katika bendi hiyo alipata ujuzi
zaidi kutoka kwa Abuu Semhando 'Baba Diana', ambaye kwa sasa ni marehemu,
ambapo anamkumbuka kwa ujuzi aliomwachia.
"Tangu 2006 nilipotua nimeweza kushiriki kupiga albamu zote na 2008 aliniachia nyimbo tano kati ya saba. "Kwa kweli Mwenyezi Mungu ailaze roho ya baba yangu Abuu Semhando mahali pema peponi, hakika bado namkumbuka kutokana na mchango wake kwangu kwa jinsi alivyokuwa akinishauri na kunipa muongozo ambao unanipa mwelekeo mzuri katika fani hii," anasema Kibosho ambaye ni mdogo wa mpiga 'drums' wa bendi ya Extra bongo, Martini Kibosho.
"Tangu 2006 nilipotua nimeweza kushiriki kupiga albamu zote na 2008 aliniachia nyimbo tano kati ya saba. "Kwa kweli Mwenyezi Mungu ailaze roho ya baba yangu Abuu Semhando mahali pema peponi, hakika bado namkumbuka kutokana na mchango wake kwangu kwa jinsi alivyokuwa akinishauri na kunipa muongozo ambao unanipa mwelekeo mzuri katika fani hii," anasema Kibosho ambaye ni mdogo wa mpiga 'drums' wa bendi ya Extra bongo, Martini Kibosho.
Kibosho anavutiwa zaidi na mpiga 'drums' Peter
Col wa Werrason Ngiama ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na malengo yake ni
kuanzisha bendi yake mwenyewe.
HUYU NDIYE JAMES MICHAEL KIBOSHO
No comments:
Post a Comment