BM BARBERSHOP KINONDONI

Saturday, August 4, 2012

MAZAO YA AFRICAN STARS OMARY SESEME NA RASHID MWEZINGO - WANATAMTAM WATESA NA SUPER KAMANYOLA JIJINI MWANZA

Omary Seseme - Mwanatamtam (African Revolution)
Mwaka 2006, wanamauziki kadhaa wa zamani walijikusanya na kuanzisha bendi ambayo ilijulikana kama Tanza Muzika. Bendi hii ilikuwa na wanamuziki kama akina Kasongo Mpinda Clayton, Issa Nundu, Mukumbule Parashi na wengine wengi wazuri. Pamoja na kuwa bendi nzuri walikosa vyombo na hivyo kuwa chini ya himaya ya jamaa walioweza kuwa na vyombo ambao nao mwaka 2007 wakajitoa na hivyo kundi hilo likavunjika.
 
 Roy Mukuna na Rashid Mwezingo - Mwanatamtam African Revolutions 

Baada ya kuvunjika kwa kundi hilo baadhi ya Wanamuziki walihamia Mwanza na kuungana na  kundi la Mwanza Carnival ambao ni pamoja na Roy Mukuna, Mukumbula Parashi, Issa Nundu, Bonny Chande na Omary Seseme. Miezi michache baadaye mfadhili wa kikundi akaanza kuugua na hivyo kundi hilo kusambaratika tena. Wanamuziki wakaamua kurudi Dar Es Salaam na kulikopelekea kujiunga kwa mkongwe mwingine ndugu Ally Yahaya, ambaye ni mpiga trumpet  na kujipa jina jipya Super Kamanyola. 
ANNA MWAOLE
 Benno Villa Anthony


Band ilipata mwaliko kwenye bonanza la Villa Park Mwanza na baada ya hapo uongozi wa Mwanza Villa Park ukaingia katika makubaliano ya  kuifanya Super Kamanyola kuwa resident Band. May 2010 bendi ikahamia rasmi Mwanza. Wanamuziki wanaounda kundi hili ni pamoja na; 
 
1. Roy Mukuna, Saxophonist na Kiongozi wa Bendi,
2. Ally Yahaya Trumpetist na Katibu wa bendi, 
3. Seseme Omary Solo guitar na uimbaji, 
4. Beno Villa Anthony mwimbaji na mpiga Keyboards na mshauri wa bendi,
5. Mukumbule Parashi muimbaji, 
6. Rashid Mwezigo mwimbaji, 
7. Anna Mwaole muimbaji, 
8. Bonny Chande Bass guitar, 
9. John Hamisi rhythm guitar, na 
10. Duncan Matembe Drums. 
 
 Ally Yahaya na Roy Mukuna
Bendi hii inakumbusha mbali sana kwa kupiga miziki ya bendi mmbalimbali zikiwemo za Maquis, OSS, Tancut Almasi, TP OK Jazz, African Fiesta n.k

No comments:

Post a Comment