BM BARBERSHOP KINONDONI

Tuesday, September 4, 2012

MTAZAMO WA SWALEH MUDHIHIR WA TANURU LA FIKARA

HUU NI MTAZAMO WANGU:

KIFO CHA MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN LIWE NI FUNDISHO KWA WAANDISHI NA VYOMBO VYA HABARI VYA TANZANIA KWA UJUMLA.

NA HAMUPASWI KULALAMIKA KWA KILICHOTOKEA BALI MUJIPONGEZE KUWA SASA MNAANZA KUVUNA KILE MLICHOPANDA NA KUPALILIA KWA MIAKA MINGI HAPA TANZANIA.

Sina maana kwamba nimefurahi kwa kile kilichotokea kule Nyololo Mufindi kufuatia kifo cha Mwandishi wa Habari na Mwakilishi kituo cha Channel 10, ndugu Mwangosi la! Hata mimi nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kwa hiki kilichotokea.

Lakini naomba niseme kwamba, kwa muda mrefu baadhi ya wananchi wa Tanzania wamekuwa wakililalamikiajeshi la Polisi kwa vitndo vyake vya mauaji na uonevu mbalimbali kwa raia. Lakini cha kusikitisha na kushangaza utakuta vyombo hivihivi vya habari ambavyo ndivyo tunavitegemea katika kutupasha habari ndivyo vinakuwa mstari wa mbele katika kulitetea jeshi la polisi na kueneza propaganda mbalimbali dhidi ya raia.
HEBU KUMBUKENI KWA HII MIFANO MICHACHE:-
1. MAUAJI YA WAISLAMU MWEMBECHAI 1998. Bilashaka wale waliopigwa, kuteswa na kuuawa waliitwa ni wahuni na vyombo vya habari vilikuwa mstari wa mbele katika kulitangaza hili.

2. KUPIGWA, KUTESWA NA KUUAWA KWA BAADHI YA WAFUASI WA CHAMA CHA CUF KUFUATIA MAANDAMANO YA JANUARI 2001 KULE ZANZIBAR. Je, vyombo vyetu vya habari viliripoti vipi taarifa hizi?

3. KUKAMATWA KWA MHADHIRI (HAMISI DIBAGULA) ETI KWA SABABU AMEITUKANA DINI NYINGINE KWA KUSEMA YESU SI MUNGU. NA WAISLAMU WALIPOAMUA KUANDAMANA KUPINGA HATUA HII, JESHI LA POLISI LILIINGILIA KATI NA WAISLAMU WENGI KUPIGWA NA KUTESWA. Vyombo vyetu vya habari vilinyamaza kimyaaaaa na kushangilia kile ambacho polisi wamefanya.

HUENDA HAYO MTAKUWA MMEYASAHAU, NAOMBA NIWAKUMBUSHE AMBAYO YAMETOKEA HIVI KARIBUNI:-
4. KULE MKOANI MOROGORO PINDI WAISLAMU WALIPOANDAMANA KUPINGA KUSIMAMISHWA MASOMO KWA WANAFUNZI WA KIISLAMU KATIKA SHULE YA NDANDA. Je, polisi walifanya nini kama si kuwapiga na kuwaonea waislamu wale walioandamana? Je, vyombo vya habari viliripoti vipi jambo hili kama si ushabiki na kueneza propaganda dhidi ya waislamu wale?
5. HEBU ANGALIENI YANAYOWAKUTA NDUGU ZETU HUKO ZANZIBAR KUTOKA JESHI LA POLISI KWA KISINGIZIO NI KIKUNDI CHA UAMSHO NA HIVI JUZI IKAWA SENSA. Hebu tazameni vyombo vya habari jinsi vinavyoripoti taarifa hizi kama si kuwaponda Waislamu na kulifagilia jeshi la polisi. Ilifikia hatua mpk gazeti fulani kubandika picha ya maandamano ya Morogoro kwa mgogoro wa Zanzibar ili kuendeleza chuki na Propaganda dhidi ya Uislamu na Waislamu.

6. BILASHAKA MNAKUMBUKA KILICHOTOKEA KWA NDUGU ZETU WA TANDAHIMBA-MTWARA, POLISI WALIPIGA RAIA, NA INASEMEKANA WALICHOMA MOTO SOKO, MADUKA YA RAIA, LAKINI CHA KUSIKITISHA ZAIDI HATA ILE OFISI YA OCD ILICHOMWA MOTO NA POLISI ILI KUPATA SABABU YA KUENDELEZA KIPIGO KWA RAIA. Lakini cha kusikitisha vyombo vya habari vilijua vyenyewe namna vilivyoripoti taarifa hizi, lakini zaidi ni kulitetea jeshi la polisi kwa kile kilichofanya.

7. JE, KUNA MAMBO MANGAPI MAZURI YA WAISLAMU VYOMBO VYA HABARI VINAAMUA KUYAKALIA NA YALE YA PROPAGANDA NDIYO YANAYOPEWA KIPAUMBELE.

Kwa hayo machache naomba niseme tena kwamba vyombo vya habari mtambue kuwa "SIMBA AKIKOSA NYAMA, HATA NYASI HULA", "UKIMUONA MWENZIO ANANYOLEWA ZAKO TIA MAJI"
Au mlisahau kuwa hata mbwa wa kumfuga mwenyewe anaweza kukujeruhi?
AU MLIDHANI KWAMBA MKIPANDA MWAROBAINI MTAVUNA TENDE???

Kimsingi, nina mengi ya kusema lakini naomba niishie hapa. ila niseme kwamba "KILICHOTOKEA NI MATUNDA YA DHULMA ILIYOPANDWA NA JESHI LA POLISI NA KUPALILIWA NA NINYI VYOMBO VYA HABARI TANGU MIAKA MINGI HAPA TANZANIA HUSUSANI KWA WAISLAMU WA TANZANIA".

By Mzee Habajana

No comments:

Post a Comment