BM BARBERSHOP KINONDONI

Monday, September 3, 2012

THE GREAT KILUVIA YAANDAA SURPRISE KWA TWANGA PEPETA

LULU KILUVIA AND REHEMA KILUVIA "THE GREAT KILUVIA"
KUPAZA SACCOS NA KALALA JUNIOR
KAMATA MPUNGA BABA
LULU KILUVIA AND REHEMA KILUVIA "THE GREAT KILUVIA"
Hakuna asiyefahamu kuwa Familia ya Kiluvia ni wadau wakubwa kwenye Tasnia ya Muziki kwa miongo mingi sasa. Jina la Kiluvia si jina geni kwenye ulingo huu wa MIZIKI hapa Bongo. Wadada wawili ambao ni vigumu kuwakosa kwenye Albam za nyimbo nyingi za Band tofauti tofauti Lulu Kiluvia na Rehema Kiluvia wameandaa Show Maalum ya kutoa shukurani kwa Wadau wa Miziki TEGETA Dar es Salaam. Usikose wewe Mtu.

Familia ya kizazi cha muziki "THE GREAT KILUVIA'S" inakuletea THE NIGHTY OF KILUVIA’S IN TEGETA. Show hii ni maalum kabisa chini ya udhamini Kampuni ya  "AMON'S COLLECTION" burudani itatolewa na The African Stras Twanga Pepeta Ijumaa hii 07/09/2012 Ukumbi wa BM Complex NDANI YA TEGETA. 

Onyesho hili ni maalum kabisa kwa wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vya jirani kuanzia Kivukoni hadi Mabwepande, Kongowe hadi Kiluvya na maeneo yoote ndani ya Jiji hili. Tumezoe kula Ubwabwa wa Mafuta kila siku sasa twende tukale Ubwabwa wa Nazi pamoja pembeni ya Bahari ya Hindi ndani ya BM COMPLEX pale TEGETA hakuna kukosa hii mambo badilisha upepo achana na hewa chafu za katikati ya Mji kila siku. Achana na kucheza Muziki kwenye Parking za Magari utaathirika na Oil na Pollution nyingine nyingi za Chemically Twende TEGETA bwana. 

Kiluvia’s wameahidi kuwepo kwa Tukio la kushitukiza ambalo litawashangaza wengi njoo uone….

No comments:

Post a Comment