Safari ya Muziki inahitaji
Uvumilivu wa hali ya juu sana. Muziki wa Dansi umeingia katika hatua nyingine
kwasasa baada la wimbi la Wanamuziki kuamka usingizini na kulilia Maslahi kwa
faida ya maisha yao. Ni kweli kuwa huwezi kufanya kazi mahali ambapo hakuna
maslahi, lakini pia huwezi kuwa na maslahi yasiyo na TIJA kwenye Kazi yako.
Lilia maslahi na fanya kazi
ionekane. Roma ni mji mkuu na mashughuli sana nchini Italia lakini haukujengwa
kwa siku moja. Kuna dhana nzuri ambayo kwasasa imeenea kwenye vinywa vya kila
Mwanamuziki kulilia maslahi. Wadau makini waliona kweli saa ya Ukombozi kwa
wanamuziki sasa imefikia mahali pazuri sana. Kibaya zaidi ni pale ulaghai unapopenya
kwenye NYOYO za wale wanaoona kuwa muziki utakuzwa kwa Pesa bila Vipaji.
Usajili wa aina yoyote unaozingatia biashara au Faida haufanywi bila Mipango.
Hakuna biashara ngumu kama ya Muziki au Mpira, unapojiingiza kwenye biashara
hizi nilazima ujipange sana na ujue kuwa kuna kukosa na kupata na huwezi kupata
faida kabla ya miaka minne hadi mitano ya KUKUBALI kupoteza hasa ukiwa umeingia
kwa DHANA ya FEDHA.
Unapokuwa na fedha na ukaonyesha
WALAFI kuwa FEDHA ipo kila mtu takuwa rafiki yako na watatokea MAGUNDI wa
kukufundisha jinsi ya kutumia FEDHA yako uliyoitafuta Mwenyewe. Hivi inakuwaje
wewe ufundishwe kutumia Fedha ambayo uliitafuta mwenyewe??? Kila mtu ana njaa
hivyo atatafuta jinsi ya kumfanya mwenye Fedha atoe pesa yake kwa Ulaghai ili
afaidi yeye.
Maneno yangu yanaweza yakawa SUMU
au CHACHU kwa wale wenye uelewa wa mbali. Kwa biashara kubwa kama hii ya Muziki
inayowahusisha watu ambao tayari wanaijua kazi yao ni ngumu sana hasa pale
wanapojazana kwa dhana ya kutengeneza pesa zaidi kuliko kazi.
SWALI NAULIZA:
Hivi uwekezaji wa Mamilioni ya
Fedha yanayosimamiwa na mtu aliyeishia Darasa la Saba ambaye hata kuhesabu moja
mpaka kumi anajifikiria mara kumi inawezekana kweli ukampa jukumu la kusimamia
mamilioni yako wakati hata neon :BUSINESS PLAN” halijui?? Naogopa sana na
ninachelea kusema kuwa nyie mliojaaliwa na Mungu kupata fedha zenu na mnayo nia
nzuri ya kuwainua hawa Wasanii wa Muziki jiulizeni kuwa tangu mlipowekeza
mmeweza kurudisha japo theluthi ya mlichotoa?? Kama bado je mnatarajia kitarudi
baada ya muda gani??? Mipango hiyo ipo??? Au mnasikiliza MILUZI??/ Hamjachelewa
jiulizeni tena Miziki si lelemama.
TWANGA YAJIPANGA UPYA
KWA KUMREJESHA KALALA JR.
USIKU wa kuamkia Jumamosi katika
Ukumbi wa Mzalendo Pale Kijitonyama Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’
ilikuwa ikimkaribisha Mwanamuziki Kalala Junior ambaye aliondoka mwaka mmoja
uliopita kwenda kutafuta maisha na Bendi ya Mapacha Watatu. Baada ya kutafuta
kwa muda huo amerejea nyumbani alikokuwa Twanga Pepeta na kusema kuwa
amejifunza mengi huko nasasa ameamua kutulia fanye kazi. Jambo hili linaonyesha
kuwa huko hakuna mapya zaidi ya kutojipanga na Ukurupukaji wa Wanamuziki,. Nderemo
na vifijo kutoka kwa mashabiki vilizizima baada ya Mwanamuziki huyo kutoa
historia ya Safari yake kupitia kwenye Wimbo wake Mpya aliokuja nao
unaojulikana kwa jina la NYUMBANI NI NYUMBANI.
No comments:
Post a Comment