BM BARBERSHOP KINONDONI

Monday, October 29, 2012

GODBLESS LEMA ANATAFUTWA NA POLISI KWA KUPORA SIMU PESA NA KUSHAMBULIA


Jeshi la polisi mkoani Arusha linamsaka aliyekuwa mmbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kwa tuhuma za kushambulia mwili pamoja na upotevu wa simu pamoja na fedha. Akiongea na waandishi wa habari jijini hapa kamanda polisi Lebaratus Sabas alisema kuwa  jeshi la Polisi linamsaka Lema na wenzake ambao idadi yake hawajatajwa kwa tuhuma za kushambulia mwili wa watu wawili tukio lililofanyika Oktoba  28 mwaka huu katika Kata ya Darajambili.

Alisema kuwa jeshi la Polisi lilipokea taarifa za malalamiko  kutoka kwa watu wawili waliojulikana kwa jina la Ibrahimu Juma pamoja na Maritin Daniel wote wakazi wa darajambili kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiwa na wanzake walimvamia na kuwashambulia kwa ngumi pamoja na kuwanyanganya simu aina ya samsung yenye thamani ya shilingi laki tatu pamoja na fedha taslim kiasi cha shilingi laki mbili kisha kuondoka na kuwaacha. Alisema kuwa watu hao waliamua kutoa taarifa polisi na polisi inamsaka Lema kwa ajili ya kujibu tuhuma hizi .

No comments:

Post a Comment