BM BARBERSHOP KINONDONI

Tuesday, October 30, 2012

KUTANA NA DACOTA NDANI X-AFRICA DTV KILA JUMAMOSI SAA MOJA JIONI .. UKOMBOZI WA MIZIKI YA DANSI



Meneja wa Band ya Mapacha watatu Hamic Dacota anatarajia kuanza kurusha Kipindi cha X-Africa kuanzia Jumamosi hii kupitia Television ya DTV kila siku ya Jumamosi kuanzia saa moja usiku.

Akiongea na Mwanatanga Hamis Dacota ambaye kwa taaluma ni Mwanahabari ameamua kuanzisha kipindi hiki ili kufufua Muziki wa dansi ambao kwasiku za karibuni umeonekana kumezwa na muziki wa Bonngo Flava ambaye yeye anauita Muziki wa Kuongea na siwa Burudani. Kama kawaida ya Hamis huwa ni mcheshi na mtu wa Utani ametumia kauli Mbiu ya BACK TO MY PROFFESSIONAL.... kuonyesha kuwa haachani na Umeneja wa Mapacha Watatu la Hasha ila ameona ni vyema pia akatumikia Taaluma yake ya Utangazaji kupitia Kipindi hiki ambacho kwasasa ni Gumzo la Jiji.

Dacota amenukuliwa na mwanatanga akisema kuwa “Najua nini mnahitaj na kwa muda mrefu mlikosa mtu wa kuwapa burudani hizo, hakuna bongo flava humu ambazo wanazilazimisha watangazaji wengine kuita muziki wa africa..hapa ni band za Tanzania ..congo..Coupe de kale Africa Magharibi kina Yousoundour..Manu Dibango wes, djako..keita..yaani wenge kofie,f ally werason, jb and many more bila kusahau zile classic swedeswede....”

Mdau mmoja maarufu bwana Gerald amemuasa Dacota kwa kusema kuwa “ Ukweli sisi walaji tunahitaji ladha mpya na nzuri ambayo tumekuwa tukiikosa kwa muda mrefu naamini Dakota umejipanga vizuri na tambua tuna mategemeo makubwa kutoka kwako...bro Mwanatanga na kubaliana na wewe kabisa kuwa muziki wa kiafrica sasa utakuwa umepata muarobaini...tuko bega kwa bega kuhakikisha X-africa inakuwa moto....

Aidha Dacota alitania na kusema ”Kaka deo ww ni mdhamini mkuu wa kazi yangu najua upokifua mbele kunilinda kunisemea..ahadi yangu kwako sintokuangusha nakuahidi mabadiliko na balance to perfection kwa kazi yooote ..kila kikundi mwanamuziki ana haki sawa hakuna upendeleo..nipo kikazi zaidi tuombe uzima show itakua kila jumamosi saa moja jioni ..kuna vipengele vitatu muhimu ..interview na wadau wa burudani ya kiafrica..interview na ma dancerz tu wake kwa waume..na wanamuziki ama band kwa ujumla ..habari za nini kinachoendelea katika tasnia hii ya muziki wa kiafrica. Yaani dance..coupe de kale..miduara,, na kila aina ya muziki wa kiafrica bongo flava haihusiki kabisa..uchambuzi wa kina ..mambo mengi mazuri mtayaona tusubiri tafadhali!!!.

Mwanatanga inaishi kwa kuamini kuwa huyu Dogo anaweza kuwa Mkombozi wa Miziki ya dansi.l


No comments:

Post a Comment