
Mkurugenzi wa ASET mama Asha Baraka anasema,
Semhando ni mwanamuziki ambaye amechangia mafanikio ya bendi hiyo kwa asilimia
kubwa kupita kiasi kutokana na kujitoa muhanga na ndiyo maana amekaa kwa muda
mrefu tangu ajiunge na Twanga Pepeta mwaka 1998 akitokea bendi ya Diamond
Sound. “Abuu aliitumikia Twanga kama mali yake binafsi! Kifo cha Semhando kilinitia
simanzi mimi binafsi na wapenzi wote wa Twanga Pepeta ndani na Nje ya Nchi. “Kwangu
Semhando alikuwa ni chachu ya mafanikio ya albamu zote 10 ambazo tumezitoa
kutokana na kushiriki katika kuandaa muziki na kusimamia nidhamu ya bendi jambo
ambalo limezidi kutupaisha katika mafanikio kwa kweli ni majonzi makubwa kumpoteza
kutokana na kuwa kiungo katika kila jambo lililohusu Twanga Pepeta,” amsema
Asha na kuongeza: “Sidhani kama tutapata mtu mwenye uwezo aliokuwa nao
mwanamuziki huyo kutokana na kipaji cha kuongoza alichokuwa nacho, kwa kweli
tutamkumbuka sana kutokana na pengo alilotuachia kwetu ASET na medani nzima ya
muziki nchini.” Kifo chake pengine kwa wanafamilia kilimgusa sana binti yake
Sharifa ambaye siku ambayo alikuwa anatakiwa kufungishwa ndoa na baba yake
ndiyo mauti yalipomkuta na kufanya sherehe hizo kugeuka msiba. Tutaendelea
kumkumbuka Marehemu Abuu Ally Semhando sisi familia ya Baraka.
 |
MKURUGENZI WA ASET ASHA BARAKA AKITOA HISTORIA YA MAREHEMU ABUU SEMHANDO |
WASIFU WA MAREHEMU ABUU ALLY SEMHANDO “LOKASSA”
KWA MUJIBU WA ASHA BARAKA
Abuu Ally
Semhando maarufu ‘Lokassa’ au ‘Baba Diana’ ambaye alikuwa mpiga drum na Meneja
wa bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’. Abuu Semhando alizaliwa mwaka 1953 Kijiji
cha Kibanda Wialaya ya Muheza Mkoani Tanga na kufariki siku ya Jumamosi 18
December 2010,
 |
ENZI ZA ABUU SEMHANDO NDANI YA TWANGA PEPETA |
Abuu Ally Semhando "Lokassa" alianza shughuli za muziki mwanzoni mwa
miaka 1970 akiwa na Tanga International na baadaye kwenda kuasisi bendi ya
Super Matimila na Orchestra Tomatoma kabla ya kutua Safari Sound Orchestra
(OSS) na Vijana Jazz ‘ Pamba Motto’ ambapo alikuwa Katibu hali kadhalika akiwa
mwasisi wa bendi ya Tanza Muzika.
 |
ABUU SEMHANDO WA PILI KULIA WALIOKAA AKIWA NA VIJANA JAZZ PICHA KWA HISANI YA MZEE JOHN KITIME |
Abuu Ally Semhando na Mzee
Hamza Kalala ni miongoni mwa wanamuziki waanzilishi wa bendi ya Super Matimila
na ndio waliomkaribisha FanFan na marehemu Dk. Remmy Ongala; Abuu alishiriki
kupiga drums kwa kiwango kikubwa katika nyimbo nyingi ambazo ziliiletea
mafaniko bendi hiyo. Akiwa katika bendi hiyo Kasaloo Kyanga alimpa jina la
Locassa na anatajwa na Kyanga katika wimbo ‘Alimasi’ wa bendi ya Matimila. Licha
ya kuwa mpiga drums, Abuu alikuwa ni mwanamuziki mwenye kipaji kikubwa cha
uongozi wa bendi (Music Band Management) na kushiriki katika kuandaa muziki ili
kuhakikisha bendi yoyote aliyopitia inapata mafanikio jambo ambalo lilimjengea
umaarufu katika kila bendi aliyopitia.
 |
ABUU SEMHANDO WA PILI KUTOKA KLUSHOTO WALIOSIMAMA ENZI ZA SUPER MATIMILA |
Historia inaonyesha kuwa bendi alizowahi kupitia
akiwa kiongozi baada ya kuondoka kwake ziliyumba na zingine kutokomea kabisa
katika medani ya muziki wa dansi, siri ya mafanikio na kipaji hicho cha uongozi
akiwa amekufa nayo. Lakini si Matimila pekee yake hata alipokuwa na Vijana Jazz
‘Sagha Rhumba’ ambako alikuwa Katibu chini ya Hemed Maneti alikuwa mmoja
wanamuziki walioshiriki katika kuiletea mafanikio kwa miaka yote hiyo kabla ya
kujiondoa, ambapo alikua muasisi wa ‘Vijana Day’. Abuu alishiriki kwa kiwango
kikubwa kutengeneza nyimbo za Vijana Jazz akiwa na waimbaji kina Hemed Maneti,
Saidi Hamis, Fred Benjamin, Cosmas Chidumule na Kida Waziri, huku wapiga vyombo
wakiwa Kurwa Milonge, Hamza Kalala, Hassan Dalali, Aggrey Ndumbalo, Disfa
Semhando (mdogo wake), Shabaan Yohana (Wanted) na wengine wengi.
 |
MAREHEMU SULEIMANI MBWEMBWE NA MZEE HAMZA KALALA WALIFANYA KAZI NA SEMHANDO PIA
|
Akiwa na wanamuziki hao ambao ni baadhi tu ya
kundi alilokuwa nalo, walishiriki kutengeneza nyimbo kali kama ‘Bujumbura’,
‘Mary Maria’, ‘Tambiko la Pambamoto’, ‘Mundinde’, ‘Ali Hassan Mwinyi Apewe Kura
za Ndiyo’, ‘Wifi Zangu Wananinyanyasa’, ‘Penzi Haligawanyiki’ na nyingine
nyingi nzuri kupindukia ambazo zilitikisa anga ya muziki huo chini ya Hemed
Maneti (Kiongozi), Hamza Kalala (Kiongozi Msaidizi) na Abuu Semhando mwenyewe
(Katibu). Katika kudhihirikisha uwezo aliokuwa nao alipojing’atua Vijana Jazz
ndipo jinamizi na anguko la bendi hiyo lilipoanza kuinyemelea tangu hapo bendi
hiyo haijafanya vyema katika medani ya muziki nchini.
Wakimzungumzia marehemu baadhi ya wanamuziki
ambao aliwahi kufanya nao kazi ni John Kitime ambaye anasema, atamkumbuka
mwanamuziki huyo kwa ucheshi wake kwa kuwa alimpokea mjini na kumtafutia malazi
jijini mwaka 1989 wakati anajiunga na Vijana Jazz akitokea Tuncut Almasi ya
Iringa.
 |
MAREHEMU ABUU AKIWA KAZINI TWANGA PEPETA KUCHEKA NA UTANI ILIKUWA SEHEMU YA MAISHA YAKE |
Aldof Mbinga ambaye alifanya kazi na Semhando
mwanzoni mwa albamu ya kwanza ya Twanga Pepeta ya ‘Kisa Mpemba’ na ‘Jirani’
alisema Tasnia ya muziki wa dansi imepoteza jemedari ambaye alikuwa hayumbi
katika misimamo yake jambo ambalo liliiletea mafanikio Vijana Jazz akiwa Katibu
na ASET akishika wadhifa kama huo.
 |
KIDA WAZIRI "STONE LADDY ALIFANYA KAZI NA SEMHANDO VIJANA JAZZ |
Wengine waliomzungumzia marehemu ni Waziri Ally
ambaye ni mwanamuziki wa bendi The Kilimanjaro ‘Wana Njenje’ akimtaja Semhando
kama nguzo iliyokatika ghafla wakati watu wakihitaji huduma na ukongwe wake
katika muziki huku Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Muziki wa Dansi Nchini
(CHAMUDATA), Juma Ubao, akimlilia kutokana kuwa chama hicho na medani ya muziki
ilikuwa ikihitaji mchango wake wakati Ally Choki anamtaja kama mtu aliyemsaidia
kumpa uzoefu wa uongozi.
 |
ABUU SEMHANDO WA KWANZA KUTOKA KUSHOTO KWENYE MOJA YA ZIARA ZA BENDI YA TWANGA PEPETA NJE YA NCHI |
Nukuu pia ilishawahi kupata ushuhuda wa Marehemu
Isihaka Kibene, ambaye alisema, Twanga Pepeta imepoteza mpiganaji na mtawala
mahiri kutokana na kuwa kiungo katika kufanya majukumu ya kila siku ya bendi. “Huyu
jamaa ni rafiki yangu sana ambaye niliwahi kufanya naye kazi kiwanda cha
uchapaji cha Printpak miaka ya 1970, na hata alipoanza shughuli za muziki
tuliendelea kuwa marafiki; namna ninavyomjua utendaji wake wa kazi medani ya
muziki na Twanga wamepoteza kichwa muhimu sana, kwa kuwa alikuwa anafanya
shughuli za watu wengine hata kama siyo idara yake ili mradi mambo yaende
sawa,” anasema Kibene ambaye ni rais wa bendi ya Walemavu ya ‘Tunaweza’.
Huyu ndiye Abuu Semhando ambaye ameacha mke na
watoto 10 na kaburi lake lipo kijiji cha Kibanda Wilaya ya Muheza alipozaliwa.
 |
JAMES KIBOSHO MRITHI WA ABUU SEMHANDO NDANI YA TWANGA PEPETA |
ANGALIA MATUKIO YA KUMBUKUMBU ZA KIFI CHA MAREHEMU ABUU ALLY SEMHANDO TAREHE 18/12/2010
 |
MWENYEKITI WA ASET BARAKA MSIILWA MWENYE SHATI LA DRAFT ALIFIKA ENEO LA TUKIO KUJIRIDHISHA... HAKUAMINI
|
 |
GARI LILILOSABABISHA MAUTI YA ABUU SEMHANDO
 |
PIKIPIKI ILIYOKUWA IKIENDESHWA NA MAREHEMU SEMHANDO BAADA YA AJALI
 |
LUIZA MUTU ALISHINDWA KUJIZUIA SIKU HIYO
|
|
|
| |
|
|
|
 |
KINAMAMA WALIMLILIA SEMHANDO |
 |
VILIO VILITAWALA KILA KONA |
 |
DUA KWA SEMHANDO |
 |
CHARLES BABA HAKUWA NYUMA KUHAKIKISHA KAKA YAKE ANAPUMZIKA KWA AMANI |
 |
MZEE KITIME PIA ALIFANYA KAZI NA SEMHANDO VIJANA JAZZ |
 |
DUA KWA MAREHEMU |
 |
SAID MDOE WA SCREEN MASTERS ALIKUWEPO PIA MBUNGE IDDI AZAN |
 |
WAOMBOLEZAJI |
 |
REY KIGOSI NA MAREHEMU STEVEN KANUMBA PIA WALISHIRIKI MSIBA WA SEMHANDO KWA ASILIMIA MIA MOJA |
 |
MOJA KATI YA MABANGO YA KUMUENZI ABUU SEMHANDO MWAKA 2011 |
RIP
ABUU ALLY SEMHANDO LOKASSA (Baba Diana, Baba Sharifa, Baba Zaituni, Baba
Mwanahamisi nk)
No comments:
Post a Comment