BM BARBERSHOP KINONDONI

Saturday, August 18, 2012

WATOTO WA MATOLA WATUPIA NNE SUPER 8

Ligi ya Super 8 iliyokuwa imeandaliwa na Benki ya ABC leo imefikia ukingoni na hatikaye kumpata Bingwa ambaye ni timu ya Simba. Mpira ulioanza Majira ya saa kumi kwenye Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam ulishuhudia Vipaji vipya kutoka Simba B ambavyo hakika watakuwa Wachezaji wakutumainiwa siku za Usoni. Msemaji wa Simba bwana Ezekiel Kamwaga ametanabahisha kuwa timu hiyo ambayo sasa ni mamilionea kwa kuchukua kitita kilicho cha mamilioni ya Pesa jioni ya leo.

Hizi ni taarifa za awali za kuwajuza wapenzi wa blog hii walioko ndani na Nje ya nchi hii, taarifa kamili juu ya mpambano huu ambao umemalizika kwa Timu kufungana mabao 4-3 (Simba 4 na Mtibwa 3). Juhudi za kumpata Mchezaji wa zamani wa Mtibwa na Taifa Stars aliyekuwa amejijengea Heshima wakati anastaafu Soka ambaye sasa ni kocha wa Timu ya Mtibwa bwana Meck Mekisime zinaendelea na blog yako itakujuza kwa kina pamoja na Habari kwa njia ya picha baadaye.
Hatimaye  kikosi cha pili cha mabingwa wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Simba ya jijini kimefanikiwa kutwaa taji la michuano ya BankABC Sup8R 2012 baada ya kuichapa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa mabao 4-3 mchezo uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam. Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana mabao 3-3 huku mabao ya Simba yakiwa yamewekwa nyavuni na Christopher Edward mawili na Haroun Athumani na kwa upande wa Mtibwa mabao yao yakifungwa Shabani Kisiga mabao mawili na Hasan Seif.

Bao muhimu kwa Simba ambalo limewapa ubingwa limewekwa kimiani na Edward Christopher ndani ya dakika 30 za  muda wa nyongeza. Mfungaji bora wa michuano hiyo amekuwa ni Edward Christopher aliyefunga mabao 9 na amepewa tuzo ya ufungaji bora.atu peke yake na kufikisha jumla ya mabao tisa, hivyo kujinyakulia tuzo ya ufungaji bora wa michuano hiyo na kuzawadiwa Sh. Milioni 2.Abuu Hashim ametajwa kuwa mchezaji bora wa Mashindano  na kuzawadiwa Sh. Milioni 2.5.

Simba kwa kuwa mabingwa wa michuano hiyo mipya ya BancABC imezawadiwa hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi milioni 40 nao Mtibwa Sugar kwa kuibuka washindi wa pili wamezawadiwa Hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi milioni 20.

No comments:

Post a Comment