BM BARBERSHOP KINONDONI

Sunday, September 2, 2012

HASIRA ZA KULETA DHARAU YA HABIB KONDO NA JUMA MGUNDA YAIGHARIMU COASTAL YACHAPWA GOLI 2-1 NA YANGA

Mabingwa wa kombe la Kagame Yanga jana waliilaza timu ngumu ya Coast Union ya Tanga kwa mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
 
Coast ndio waliokuwa wa kwanza kuandika bao mapema kipindi cha kwanza likifungwa na kiungo wake Razak Khalfani kwa shuti kali la mbali lililomshinda  mlinda mlango wa Yanga Ally Mustafa'Bartez'.
 
Mabao ya Yanga yalipatikana katika kipindi cha pili, la kwanza likitokana na mpira wa kujifunga baada ya krosi kali ya Shamte Ally na mchezaji Philipo kuusindikiza mpira Wavuni kwa kichwa. Bao la pili lilifungwa na Said Bahanuzi “Spider Man” kwa shuti kali lililogonga mwamba na kisha kutinga wavuni.
 
Coast walilazimika kucheza pungufu katika sehemu kubwa ya kipindi cha pili cha mchezo  kufuatia kiungo wake Jeri Santo kutolewa nje ya uwanja kwa kadi nyekundu baada ya kutoa lugha chafu kwa mwamuzi.
 
Aidha katika mchezo wa jana nusura ulsichezwe baada ya kutokea hali ya sintofahamu muda mfupi kabla ya mchezo kuanza. Sintofahamu hiyo ilisababishwa na uchelewaji wa timu ya Coastal Union ambayo iliingia uwanjani saa 10:14 na kuanza kupasha viungo wakati muda wa kufanya hivyo ulikuwa umesha kwisha. Mchezaji wa zamani wa Coastal Union Juma Mgunda ambaye ndiye Kocha wa timu hiyo pamoja na Habibu Kondo waliendelea kuwapa mazoezi wachezaji wao wakati refa alipowataka kuingia Vyumbani kwa ukaguzi.
 
Refa wa Mchezo huo aliwaita Yanga na kuingia nao uwanjani na kufanya ukaguzi kwa mujibu wa Sheria inavyotaka. Coastal waliendelea kukaidi agizo la Refa hivyo Kocha wa Yanga aliamua kuitoa timu Uwanjani na kuelekea vyumbani. Hekima ilitumika kuwashawishi Yanga kurejea uwanjani na hatimaye mpira ukachezwa.

No comments:

Post a Comment